Connect with us

Hi, what are you looking for?

News

Serikali Kuu Kuajiri Gen Z 40,000 Kaunti ya Nairobi

Na RIPOTA WETU

Alhamisi, Machi 13, 2025

ZIARA ya rais William Ruto na Naibu wake Prof Kithure Kindiki, jijini Nairobi, Jumatano, katika  eneo Bunge la Dagoretti kusini na Westlands ilikuwa ya kufana.  Rais alisema kuwa serikali yake itaajiri vijana 40,000 katika mradi wa kuzoa taka kwenye mto Nairobi, kuweka mazingira safi ili kuvutia wawekezaji nchini. 

Vijana watapewa jukumu la kuweka mazingira safi, ujenzi wa mabomba ya maji taka na ujenzi wa nyuma za bei nafuu.  Wakati huu wapo vijana 22000  katika mitaa ya Kaunti ya Nairobi wakipiga shughuli hizo kupitia agizo la Rais Ruto. Pia wengine wapatao 18,000 watapewa ajira hiyo na baadaye wengine 1000 watafuata mkondo huo.

Wakati wa ziara hiyo eneo la Dagoretti na Westlands, Naibu Rais Prof Kithure Kindiki aliwahimiza vijana wajisajili upesi kwa mradi huo wa miaka miwili akidai utawapa mwongozo wa kimaendeleo.

“Tungetaka wavulana na wasichana wapate  ajira ili waweze kujikimu kimaisha huku tukiendesha nchi mbele,” alisema Pro Kindiki.  Aliongeza kuwa wamepania tuwe na serikali ya uzalendo, umoja, ili kujenga Taifa lenye mshikamano,” alifafanua Naibu Rais.. Hata hivyo,  Rais Ruto alihakikishia wananchi kwamba Bima ya afya ya SHA, itafanyiwa marekebisho mara moja ili ifaidi kila mwananchi bila ubaguzi. “Hapo awali Bima ya matibabu ilinufaisha wanaofanya kazi na wenye Pesa, lakini wakati huu, tutahakikisha kila mwananchi anapata matibabu ,” akasema Rais. Wakati huo pia alihaidi Gavana wa Kaunti ya Nairobi, Johnson Sakaja kuwa hospitali iliyokwama kukamilika eneo ya Dagoretti kusini,  iliyotarajia kugharimu  Sh 230 milioni itakamilishwa hivi karibuni. Aliamuru wajenzi wa hospitali hiyo waanza kazi baada ya wiki mbili bila kuchelewa. Aliagiza pia ujenzi huo ung’oe nanga mwezi Aprili hadi Agosti, 2025  ili iwe imekamikika.

Naye Naibu Rais,  alisema wanatarajia kujumuisha vijana wapatao 22,000  katika miradi tofauti kama mtandao ICT na mradi wa ajira katika mataifa ya ng’ambo ili wajiendeleze kimaisha. Rais alisema miradi wa soko ya kisasa ya Riruta na hospitali ya Dagoretti itapewa kipau mbele na serikali yake. Rais alidokeza kuwa serikali imo mbioni kuona kwamba Shule ya Msingi ya Kawangware pia sekondari ya Gatina eneo la Westlands, shule ya Msingi ya Kangemi na Daraja la Kangemi zitashughulikiwa upesi. Alidokeza kuwa kuungana pamoja na wananchi ni muhimu kwa manufaa ya umoja wa  nchi.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You May Also Like

News

Na RIPOTA WETU Jumamosi, Januari 11, 2025 SHULE ya Upili ya MP Shah Chania High ya Thika, Kaunti ya Kiambu, ilifanikiwa kupata wanafunzi 22...

News

Na RIPOTA WETU Jumamosi, Januari 11, 2025 SHULE ya Upili ya Thika High inajivunia wanafunzi wapatao 25 kuandikisha alama za A na A- kwenye...

Sports

Na RIPOTA WETU Jumanne, Januari 21, 2025 TIMU ya wanaume ya Simlaw na Jacaranda kila moja ilionyesha voliboli ya kuvutia na kunasa tikiti ya...

Sports

By Our Reporter Monday, September 8, 2025  THE National Commercial Bank of Africa (NCBA) men’s football team defeated Consolidated Bank 2-0 in 39th edition...